• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi Watakiwa Kuchangamkia Fursa ya Kujipatia Kipato

Imetumwa: May 4th, 2023

Wananchi wamehimizwa kuchangamkia fursa za usogezaji wa mawe, upondaji wa kokoto katika ujenzi wa vyumba tisa vya madarasa eneo la Kikuyuni kupitia Mradi wa Boost.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Songwe Mhe. Solomon Itunda akizungumza mara baada ya shughuli ya kuchimba msingi wa kuanza ujenzi wa shule hiyo kwa kushirikiana na wananchi wa kitongoji cha Kikuyuni Kata ya Mkwajuni uliyofanyika Mei 3, 2023.

Mkuu wa Wilaya ya Songwe amesema Mradi wa Boost unatakiwa ku'boosti' hata maisha ya wananchi wa kawaida ili mbali na maboresho ya kielimu pia wananchi uchumi wao uwe bora.

Amesema ujenzi wa shule hiyo mpya yenye madarasa saba ya shule ya msingi na madarasa mawili kwa shule ya awali (mfano) wananchi wanapaswa kuchangamkia  fursa za kuponda kokoto, kusogeza mawe kwa ajili ya ujenzi wa msingi.

"Tunataka hizi hela zisitoke hapa kwetu [Songwe DC] sogezini mawe, pondeni kokoto mtapata hela na shule itajengwa ili watoto wenu wasome hapa", alisema Mhe. Itunda ambaye alikuwa ameambatana na viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songwe Ndg. Mabrouck Mwaiswelo amewasihi wananchi wa kijiji cha Kaloleni kuendelea kumuombea afya njema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kutokana na kuendelea kuigusa Wilaya ya Songwe katika miradi mikubwa ya maendeleo, akisema pongezi za kutosha ni kumpa kura za kutosha kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

CPA. Cecilia Kavishe, Mkurugenzi Mtendaji Songwe DC amewaambia wananchi kuwa Mama Samia ameipatia Kikuyuni milioni 538 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule ya awali na msingi.

CPA. Cecilia Kavishe amewahimiza wanawake kujitokeza zaidi kuponda kokoto ili waimarishe uchumi wao na familia zao.

Mwakilishi wa wananchi Kata ya Mkwajuni Mhe. Shaibath Kapingu akizungumza kwenye shughuli hiyo ameipongeza serikali ya Rais Samia huku akiomba Tarura kuwasaidia kujenga barabara ili vifaa vifike kwenye eneo la mradi kiurahisi.

Halmashauri ya Songwe DC imepokea bilioni 1.04 kupitia Mradi wa Boost kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya elimu awali na msingi, kijiji cha Kaloleni ndiyo iliyopokea fedha nyingi kulinganisha na maeneo Wilayani hapa.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.