• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

Imetumwa: May 24th, 2023

Wakulima wa Kijiji cha Magamba, Kata ya Magamba Wilayani Songwe mkoa wa Songwe wameishukuru serikali ya Halmashauri ya Wilaya ya Songwe kwa kuanzisha mfumo wa uuzaji wa zao la ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani ambao wameutaja kuwa mkombozi wa kilimo chao.

Wakulima hao kwa nyakati tofauti wamezungumza hayo baada ya kumalizika mnada wa tatu wa ufuta Wilayani Songwe huku bei zikiendelea kupaa katika kila mnada kuanzia uliofanyika Mei 5 hadi Jumatano Mei 24, 2023.

Bi. Pelegia Boniface Simfukwe, 38, akizungumza kando na ghala la Magamba ambako mnada umefanyika amesema amekuwa akilima ufuta kwa muda mrefu hajawahi kuuza ufuta wake katika bei inayokaribiana na mnada wa Leo [Jumatano Mei 24].

"Tulikuwa tunauza ufuta lakini hii bei ni nzuri kwetu wakulima, mwanzoni bei ilikuwa ikipanda sana inakuwa 2,500 hadi 3,000 lakini sasa tumeuza 3,678", alisema Bi. Pelegia akiwa amejifunga kilemba kichwani.

Christopher Yunji akizungumza baada ya mnada amesema anaipongeza serikali kwa kuleta mfumo wa stakabadhi ghala ingawa amekiri wazi kwamba mwanzoni alikuwa anahofia lakini sasa amepata uelewa wa namna unavyoendeshwa ataenda kuwahamasisha wakulima wengi zaidi.

Pongezi hizo zimetolewa pia na Willy Julius Msukwa ambaye pia ni mkulima wa kijiji cha Magamba ambaye amesema kutokana na mfumo huo anategemea uchumi wa familia yake kuimarika ambapo ameomba serikali kwa mwaka ujao kuanza masoko mapema zaidi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe CPA. Cecilia Kavishe akizungumza kwenye mnada huo amewaeleza wananchi kuwa kutokana na mfumo wa stakabadhi ghalani Halmashauri inategemea kupata takwimu sahihi za wakulima lakini pia itaanza kugawa mbegu za ufuta bure kwa wakulima kuanzia msimu ujao wa kilimo pamoja na ili kuongeza kasi katika uzalishaji.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe Mhe. Godian Wangala alimwakilisha mwenyekiti wa Halmashauri amesisitiza suala la mkulima kuwa huru kuanza ufuta wake popote pale ndani ya Wilaya ya Songwe isipokuwa mnunuzi hataruhusiwa kuuza ufuta huo bila kupitia stakabadhi ghalani.

Kuhusu minada ya mara kwa mara, Mhe. Wangala amesema kama Halmashauri wanaendelea kuratibu kuona namna ya kuboresha tarehe ya mnada mmoja na unaofuata ili kumfanya mkulima auze zao lake kiurahisi na bei nzuri.

Mnada wa Leo Jumatano, ghala la Magamba ni wa tatu kwa Songwe DC katika mkoa wa Songwe ambapo takribani tani 1555.773 sawa na kilo 1,555,773 zimeuzwa kwa shilingi 3,678.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.