• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Songwe DC Yapokea Bilioni 1.04 Katika Mradi wa Boost

Imetumwa: April 15th, 2023

Kamati Simamizi ya Mradi wa Boost ngazi ya Halmashauri ya Wilaya ya Songwe imetambulisha Mradi wa Boost ambao unaenda kuboresha na kujenga miundombinu ya elimu katika Divisheni ya Elimu Awali na Elimu Msingi kwa shule mbalimbali.

Mratibu wa Mradi Wilaya ya Songwe Ndg. Lucian Yunga akizungumza na Viongozi wa Kata ya Mkwajuni wakati wa kutambulisha Mradi huo shughuli iliyofanyika Shule ya Msingi Mkwajuni Jumanne Aprili 11, 2023 amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetenga zaidi ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa kata ya Mkwajuni pekee.

Yunga ameeleza kuwa kati ya fedha hizo, milioni 538,500,000 ni ajili ya ujenzi wa vyumba saba vya Shule ya Msingi Kikuyuni, vyumba vya madarasa viwili vya awali [Shule ya Mfano] pamoja na matundu sita ya vyoo.

Wakati huo milioni 50,000,000 zinaenda kujenga miundombinu ya vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Osterbay ambayo pia matundu matatu ya vyoo yatajengwa kwa milioni sita.

Katika hatua nyingine, Yunga amewahimiza viongozi wa vijiji kutenga maeneo ambayo ni salama kwa wanafunzi kufika shuleni lakini maeneo ambayo hayana migogoro ya wananchi kwa wananchi ama wananchi na serikali.

Mhasibu wa Mradi wa Boost ngazi ya Halmashauri, Noel Hango amewaomba viongozi wa Kata na vijiji kusimamia kwa uzalendo miradi ambayo imechaguliwa kufanyika kwenye vijiji vyao, akisisitiza umuhimu wa kutunza nyaraka mbalimbali ili kuepukana na hoja za wakaguzi wa ndani na nje ya Halmashauri.

Diwani wa kata ya Mkwajuni Mhe. Shaibath Kapingu akizungumza katika kikao hicho, amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipatia Mkwajuni milioni 600, akisema kuwa kwa nguvu za wananchi wasingeweza kuwa na shule kama ambayo itajengwa kupitia fedha za Boost.

Mradi wa Boost unatekelezwa kwa miaka mitano ambapo utakelezaji wake unategemea na matokeo yatakayopatikana kwenye ujenzi wa mwaka wa kwanza.

Wilaya ya Songwe kupitia Mradi wa Boost imepokea bilioni 1,039,600,000 ambazo zinaenda kuboresha mazingira ya elimu awali na msingi.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.