• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Msiende Na Pikipiki Hizi "Bar" - Katibu Tawala

Imetumwa: March 11th, 2023

Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Songwe Ndg. Chesko Mbilinyi amewataka Maafisa Ugani waliokabidhiwa pikipiki 19, moja kwa kila mmoja kuhakikisha wanazitumia pikipiki hizo kwa matumizi ya ofisi, wakiwafikia wakulima, wafugaji wa hali ya chini wakiachana na tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakitumia vyombo vya usafiri vya serikali kwenda kwenye maeneo ya starehe kama "Bar".

Kauli hiyo imetolewa Jumamosi nje ya Ofisi za Mkurugenzi Mtendaji zilizopo eneo la Kimborokoto wakati wa hafla ya kukabidhiwa pikipiki kwa Maafisa Ugani 19 ambazo zimeletwa ili kurahisisha utendaji kazi wa maafisa ugani hasa kwa Wilaya ya Songwe ambayo jiografia yake ni ngumu.

Ndg. Mbilinyi amewaeleza Maafisa Ugani kuwa waende wakazitumie pikipiki kama ambavyo serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekusudia.

"Wafikieni wakulima, wafikieni wafugaji zile changamoto za wafugaji kusema wanashindwa kufuga kwa sababu hawana elimu ziishe, wanufaika wa TASAF [Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini] wamekuwa wakisema hawana elimu ya ufugaji hakikisheni mnawafikia, mnawapa ushauri na elimu", alisema.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe CPA. Cecilia Kavishe akizungumza katika hafla hiyo amewaambia Maafisa Ugani kuwa washirikiane na Watendaji wa Kata na Vijiji kusimamia ukusanyaji wa mapato. 

Amesema itakuwa ajabu kama wamepewa pikipiki halafu mapato yataendelea kupotea, "tutakuwa hatutimizi lengo la Mheshimiwa Rais wetu".

CPA. Kavishe ametumia nafasi hiyo, kumpongeza Mheshimiwa Rais ambaye anaenda kutimiza miaka miwili madarakani kwa kuendelea kuwakumbuka watumishi na kuboresha mazingira ya utendaji wa kazi suala ambalo amelitaja kuwa linaongeza ari ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Andrew Kayombo, Afisa Kilimo na Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, akiongea kwenye zoezi hilo, amesema pikipiki ambazo zimepokelewa ni 19 na zimekabidhiwa kwa maafisa Ugani ambapo wale watakaoweza kuzitunza kwa muda wa miaka miwili, bodaboda hizo zitakuwa za kwao kama ambavyo maelezo ya wizara yanaeleza.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.