• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Vyumba Tisa vya Madarasa, Madawati Kwa Milioni 180 Vyakamilika, Wazazi Watakiwa Kutowaficha Watoto

Imetumwa: December 20th, 2022

Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Songwe Chesko Mbilinyi amewataka wazazi ambao watoto wao wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza 2023 kuhakikisha wanafanya hivyo kuanzia Januari Mosi 09.

Kaimu Katibu Tawala Chesko Mbilinyi ametoa wito huo wakati akikabidhiwa vyumba vya madarasa 9 vikiwa na madawati ndani kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ambavyo vimejengwa na kukamilika vikiwasubili wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023, tukio lililofanyika katika Shule ya Sekondari Kanga (vyumba vitatu na Ofisi), Sume na Namalaji.

Ndg. Mbilinyi amesema haitakuwa na maana kama vyumba vya madarasa vimekamilika lakini vikakosa wanafunzi kwa makusudi ya mzazi au mlezi.

“Ndugu zangu wazazi madarasa haya ni ya kwenu, watoto wenu wanatakiwa kusoma kwenye hayo madarasa, msiwafiche vijana wenu”. Alisema.

Pia, Kaimu Katibu Tawala huyo amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe pamoja na wataalamu kwa kusimamia vizuri ujenzi vya vyumba vya madarasa, ofisi na madawati, akisema usimamiaji huo ndiyo dhana ya uzalendo na uwajibikaji.

CPA Cecilia Kavishe, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe akizungumza baada ya kukabidhi vyumba vya madarasa na madawati vilivyokamilika kwa asilimia 100 kwa Kaimu Katibu Tawala ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha milioni 180 kwa ajiili ya ujenzi wa madarasa tisa, madawati na ofisi katika shule ya sekondari Kanga.

“Leo (Disemba 20, 2022) ni siku ya kipekee kwani tunakabidhi madarasa, madawati na ofisi vikiwa vimekamilika. Tunampongeza sana Mhe. Rais kwa kutuletea fedha hizi wananchi wa Songwe, wanafunzi 450 siyo wachache wanaotarajia kuanza kuyatumia madarasa hayo”. CPA Cecilia alitoa pongezi hizo akiwa katika Shule ya Sekondari Kanga.

Mwakilishi wa wananchi kata ya Kanga Mhe. Erick Kihinda amesema ujenzi wa vyumba vya madarasa vitatu na ofisi katika kata yake itaenda kuongeza imani ya wananchi kwa viongozi wao, wataona serikali imethamini kwani watoto wao hawatasoma kwa shida tena.

Jumla ya wanafunzi 2,364 wanategemea kuanza masomo ya kidato cha kwanza wilayani Songwe kwa mwaka 2023 ambapo kati ya wanafunzi hao, 450 ikiwa na maana ya wanafunzi 50 kwa kila darasa watatumia madarasa hayo mapya ambayo yamejengwa kwa fedha maarufu kama “Pochi la Mama”.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.