• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Vijana Bodaboda Watakiwa Kujiepusha na Ajali

Imetumwa: April 5th, 2023

Wanufaika vijana wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Songwe wametakiwa kuchukua tahadhari katika namna ya kuendesha pikipiki ambazo wamekabidhiwa ili waepukane na ajali ambazo zinazaweza kujitokeza kutokana na uzembe wa kutokuwa makini barabarani.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe Mhe. Abraham Kaguluka Sambila wakati akikabidhi pikipiki 47 kwa vikundi 9 vya vijana zenye thamani ya shilingi milioni 123,140,000 kutokana na mapato ya ndani, shughuli iliyofanyika nje ya Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji iliyopo Kimborokoto, Mkwajuni Aprili 06, 2023.

Mhe. Sambila amesema pamoja na lengo la serikali la kuwanufaisha vijana kiuchumi lakini mikopo itakosa maana kama vijana ambao wamekopeshwa hiyo mikopo wataishia kuwa wenye ulemavu kutokana na madhara ya kutotumia vizuri pikipiki kwa kuzingatia taratibu za barabarani.

“Lakini kubwa kuliko ni usalama wenu, pikipiki hizi zitakosa maana kama mtaishia kuwa walemavu. Vijana wangu, pikipiki zinaua, mkishindwa kuwa waangalifu wa kufuata sheria za barabarani mtakuwa walemavu na sisi Halmashauri tutakuja kukudai tu na ulemavu wako, kwa hiyo nendeni mkawe waangalifu”, alisema Mhe. Sambila ambaye ni Diwani wa Kata ya Mbangala.

Diwani huyo pia amewaeleza vijana kuwa, Halmashauri ya Wilaya ya Songwe itaendelea kukopesha mikopo kwa makundi yote kama ambavyo serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ikiagiza lengo likiwa ni kuwapa ajira na kuwapa uchumi mzuri wananchi wake kupitia mikopo hiyo isiyokuwa na riba.

 “Tutaendelea kutoa mikopo kama ambavyo tunaelekezwa. Lengo mpate ajira maana siyo lazima uje hapa ofisini ndiyo ujione kama umeajiriwa, pikipiki ni ajira kama zilivyo ajira nyingine”, aliongeza.

Abdallah Mgonja, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe amewahimiza vijana kuwekeza nguvu kubwa katika marejesho ili waweze kumaliza mapema wabakie na umiliki kamili wa pikipiki angalia zikiwa mpya.

“Tunategemea nyinyi baada ya hapa mtaanza kazi rasmi na mapato yenu kipaumbele cha kwanza inatakiwa mfikirie kufanya marejesho, bora mjinyime saizi mfanye marejesho haraka ili muwe huru na pikipiki zenu wenyewe”, alisema Mgonja, Mtaalamu wa Misitu na Maliasili.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mikopo ya Halmashauri ya wilaya ya songwe, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Thomas Kiwoi amesema kwa mwaka wa fedha 2022-2023, Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ilipanga kukopesha shilingi milioni 304,480,000 ambapo katika robo ya tatu [Januari–Machi] Halmashauri ya Wilaya ya Songwe imeshakopesha jumla ya shilingi milioni 175,74,500 na kwa kundi la vijana wamekabidhiwa vijana pikipiki 47 shilingi milioni 123,140,000.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.