• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Stakabadhi Ghalani Imekuja Kutuinua Wakulima- Wangala.

Imetumwa: January 12th, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe amewasihi wakulima wa kilimo cha ufuta Wilayani Songwe wajiunge na vyama vya ushirika ambavyo vitawasaidia kuwa na kilimo chenye tija na manufaa kwao na Halmashauri.

Mhe. Wangala amesema hayo wakati wa ziara ya kutembelea kata za Bondeni, Tarafa ya Songwe kutoa elimu na kuhamasisha wakulima wa ufuta kujiunga na vyama vya ushirika ambavyo utawafanya kuwa pamoja na stakabadhi ghalani ndiyo itakuwa suluhisho la upatikanaji wa bei nzuri, pembejeo za kilimo, ushauri wa kitaalamu sambamba na kupata mikopo yenye riba nzuri.

Akiwa ameambatana na Watalaamu wa kilimo na ushirika kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Songwe, Mhe. Wangala ameongeza kuwa mateso ambayo wakulima walikuwa wanapata wataachana nayo kwa kujiunga na ushirika na stakabadhi ghalani.

"Serikali imeona (wakulima) tunaonewa,  bei zinakuwa mbaya, mikopo wanatupa haina afya kwenye ustawi wetu, sasa wametuletea stakabadhi ghalani, tujiunge wakulima wenzangu", alisema Mheshimiwa Wangala akizungumza kata ya Mpona.

"Niwaambie sisi tumeenda kujifunza kwa wenzetu wa Lindi wanavyofanya, tumeona mfumo huu (stakabadhi ghalani) ni mkombozi wetu kwa sababu bei ya ufuta wetu itakuwa na ushindani lakini pia tutakuwa na bima endapo majanga yatatokea", alisema Mhe. Wangala akimuwakilisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Songwe Mhe. Abrahamu Sambila.

Diwani wa kata ya Manda Mhe. Joseph Maige Machumu ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya uchumi, ujenzi na mazingira akizungumza na wananchi wa Kata ya Mpona na Totowe amewasihi wananchi hao kutumia vizuri uhuru wa kujiunga na vyama vya ushirika kwa kuamua kujiunga navyo kwani wakulima watakao kuwa wamejiunga wataweza kuhifadhiwa ufuta wao na kuwauzia bei nzuri ambayo wanunuzi wameshindana tayari.

Mhe. Maige amewasihi wakulima ambao watakuwa tayari kuingia kwenye vyama vya ushirika kuhakikisha wanachagua viongozi imara ambao watakuwa na uwezo wa kusimamia mahitaji ya wakulima.

Afisa Ushirika wa Halmashauri David Mbembela akiongea wakati wa kutoa hamasa hiyo amesema vikundi vya ushirika vinatakiwa kuwa na watu angalau 30 au kuendelee ambapo kwenye vikundi hivyo kutakuwa na viongozi ambao watawaongoza wengine.

Kaimu Afisa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Wilaya Andrew Kayombo amesema pamoja na kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani utarahisisha ukusanyaji wa mapato kwa Halmashauri lakini pia mfumo huo utawapa wataalamu wa kilimo urahisi wa kwenda kutoa elimu ya kilimo.

Ziara ya kutoa elimu kwa wakulima wa ufuta kwa kata za bondeni awamu ya kwanza imeshafika kata ya Totowe, Namkukwe, Mpona na Manda.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.