• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

"Kuweni Mabalozi wa Amani"

Imetumwa: November 20th, 2022

Wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la Akiba Kata ya Udinde Wilayani Songwe mkoani Songwe wametakiwa kutumia mafunzo waliyopata ya kizalendo kutunza amani na utulivu ya wananchi wa Songwe na taifa kwa ujumla.

Wahitimu hao 85, wakiume 62 na wanawake 23 wamepewa agizo hilo na Mkuu wa Wilaya ya Songwe ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi wa hafla hiyo Mhe. Simon Simalenga amesema hayo wakati akifunga mafunzo yaliyofanyika kwa miezi minne katika Kata ya Udinde.

Mkuu wa Wilaya ya Songwe Mhe. Simalenga amesema mafunzo waliyopata wahitimu hao kuwa chachu katika kujua namna ya kuilinda na kuitetea nchi.

Amesema itakuwa ajabu kama watu waliopata mafunzo wanajihusisha na uhalifu badala ya kutunza amani, kuchochea ugomvi badala ya kuwa sehemu ya kimbilio kutokana na uzalendo mliofundishwa.

"Aaah sitaki kusikia habari za uhalifu hapa, nataka muwe chanzo cha amani" alisisitiza Mkuu wa Wilaya.

Pia, wahitimu wametakiwa kutumia elimu waliyoipata katika kujiingiza katika shughuli za kuzalisha ili waweze kuwa na kipato chao wenyewe.

Chesko Mbilinyi, Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Songwe amewahimiza wahitimu wa mafunzo hayo kushiriki katika kampeni ya kuzuia uvuaji haramu wa samaki Ziwa Rukwa, "najua wengi wanaovua kwa kutumia nyavu zisizo rafiki kama kokoro na timba siyo wenyeji wa hapa (Udinde), wakomesheni hao".

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe CPA Cecilia Kavishe akizungumza katika siku ya hitimisho la mafunzo ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza katika kata ya Udinde tangia mwaka 1999 amesema atawaelekeza wataalamu wa maendeleo ya jamii wa Halmashauri kutenga muda kuja kuwafundisha juu ya mikopo ya 10% ili wale watakaokuwa na uhitaji na sifa wapatiwe mikopo kwenye kundi la vijana.

Mafunzo hayo hufanyika kila mwaka ambapo Frank Cibaya, Mkuu wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Songwe akisoma taarifa ya mafunzo hayo alisema kuwa wanafunzi walianza 216; 25 (23) katika idadi hiyo walikuwa ni wanawake.

Matangazo

  • HAYA HAPA MAJINA YA WANANCHI WALIOPATA VIWANJA ENEO LA KALOLENI NA SAZA October 03, 2022
  • TANGAZO LA KAZI YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI II SONGWE DC April 03, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI November 11, 2022
  • WANAHITAJIKA MAFUNDI UJENZI SONGWE DC December 07, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Siku ya Mazingira Duniani 2023: Utunzaji wa Mazingira Wasisitizwa Wilayani Songwe

    June 05, 2023
  • DC Songwe Ataka Taasisi Za Serikali Zihusishwe Kwenye Ujenzi wa Miundombinu

    June 02, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Magamba Waishukuru Halmashauri ya Songwe kwa Kuanzisha Stakabadhi Ghalani

    May 24, 2023
  • ALAT Yaipongeza Songwe DC Kwa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kisasa

    May 05, 2023
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.