• Maswali |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
Songwe District Council
Songwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Tehama
      • Ukagazi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma Za Maji
  • Madiwani
    • orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha,Mipango na Utawala
      • Kamati ya Elimu Afya Na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Kikao cha madiwani
      • Meeting With Chairman Of Council
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Utangulizi
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fom ya Maombi
    • Utangulizi
    • Mpango Kazi
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Kilichoongelewa
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DED Songwe Asherekea Kuzaliwa Kwake na Wanafunzi wa Sekondari Kapalala.

Imetumwa: November 13th, 2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe CPA Cecilia Kavishe ameitumia Siku ya Kumbukizi ya Kuzaliwa kwake (Octoba 29) kwa kushiriki chakula cha mchana na kukata keki pamoja na Wanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kapalala ambayo iko Tarafa ya Kwimba.

Mkurugenzi Mtendaji CPA Cecilia ameshiriki tukio hilo Leo Jumamosi Novemba 13, 2021 ambapo ametumia wasaa huo kuwahamasisha Wanafunzi wafanye vizuri na waondoa hofu wakati wote watakaokuwa kwenye vyumba vya mitihani hali kadhalika katika maandalizi ya mwisho.

Amesema hakuna mbadala wa elimu, hakuna haja ya kuwa na hofu, akiwataka kila mmoja kutambua kuwa miaka minne ambayo wamekaa shuleni siyo hivyo wajitahidi kufanya vizuri kwenye mitihani wa mwisho ambayo utakuwa urithi wao wenyewe na fahari kwa wazazi na walezi.

Aidha, CPA Cecilia amewashukuru Wazazi/Walezi kwa kuwasimamia watoto wao kuhakikisha wanahitimu masomo mbali na changamoto kwa baadhi ya wanajamii kukosa mwamko wa elimu.

Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Kapalala Raimos Benson Mwashilindi akizungumza kwa niaba ya Waalimu na wazazi amempongeza Mkurugenzi Mtendaji CPA Cecilia, akisema zawadi aliyoitoa kwao ya kushiriki sherehe ya kuzaliwa na Wanafunzi ni tukio kubwa na la kipekee hasa ikiwa Shule hiyo haikufanya mahafali.

"Mama tunakupongeza, maana una Shule nyingi Wilayani hapa, ungeamua kwenda kula keki sehemu nyingine lakini umekuja hapa, Mungu akubariki", alisema Mwashilindi katika sherehe hiyo fupi iliyofanyika katika moja ya darasa shuleni hapo.

Naye, Rose Mwakalindile, Kaimu Afisa Elimu Sekondari ametoa pongezi kwa Mkurugenzi Mtendaji ambapo pia amewasihi Wanafunzi kuendelea kujisomea mpaka siku ya mwisho akisema kwenye elimu Ng'ombe hunenepa siku ya mnada tofauti na usemi wa wahenga.

CPA Cecilia Kavishe aliamua kula chakula cha mchana na kukata keki pamoja na Wanafunzi hao ikiwa ni sehemu ya kutakia kheri.

Jumla ya wanafunzi 28 wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kapalala wanategemea kuanza mitihani ya kuhitimu masomo yao siku ya Jumatatu Novemba 15, ambapo Wanafunzi wa kike ni watatu (3) pekee.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU March 23, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • TANGAZO

    March 13, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    February 14, 2022
  • Silinde Apongezi Kasi, Ubora wa Majengo ya Uviko-19 Songwe.

    November 22, 2021
  • DED Songwe Asherekea Kuzaliwa Kwake na Wanafunzi wa Sekondari Kapalala.

    November 13, 2021
  • Ona Zote

Video

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VIRUSI VYA CORONA
Ziada Video

Kurasa za Karibu

  • PReM
  • PlanRep System
  • FFARS System
  • STMIS system
  • Mfumo wa kuomba ajira za walimu kwa njia ya mtandao
  • Tovuti ya kuomba Ajira Serikalini

Viungio Vinavyoshabiana

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • e-Government Agency
  • Ofisi ya Rais IKULU
  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali ya Tanzania
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe

Watazamaji Duniani

world map hits counter

Watazamaji Wageni

Dissertation-WritingService.com

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mkwajuni-Kimborokoto - Saza Road

    Anuani ya Posta: P.o.Box 77 Mkwajuni Songwe

    Mawasiliano: +255 (025) 2520301

    Simu: +255 (025) 2520301

    Barua Pepe: ded@songwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera Binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma Zetu

Copyright ©2020 Songwe District Council . All rights reserved.